MSIKILIZE MUUMIN AKIZIKOSOA TUZO TATU ZA MUZIKI WA DANSI ZILIZOTOLEWA KWA JOSE MARA, FERGUSON NA MASHUJAA BAND

Mwimbaji nyota wa muziki wa dansi, Mwinjuma Muumin.

MWIMBAJI nyota wa muziki wa dansi, Mwinjuma Muumin amezikosoa tuzo tatu za muziki wa dansi zilizotolewa Jumamosi, Mlimani City katika usiku wa tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards.

 Muumin alitoa tathmini yake jana mchana katika ofisi za Saluti5 ambapo alisema hakubaliani na Mashujaa Band kupewa tuzo ya bendi bora ya mwaka, hakubaliani pia na Jose Mara kuwa mwimbaji bora wa mwaka huku pia akishangaa Ferguson kuwa rapa bora wa mwaka.

Mwimbaji huyo ameshangaa bendi kama FM Academia au Twanga Pepeta kukosa tuzo ya bendi bora, lakini akashangaa zaidi Jose Mara anakuwaje mwimbaji bora mbele ya mtu kama Christian Bella halafu Ferguson ampiku Totoo ze Bingwa au Kitokololo.  

CHANZO SALUTI5


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo