INASIKITISHA: MWANAMKE AUAWA KINYAMA KWA KUCHINJWA WILAYANI ROMBO MKOANI KILIMANJARO

Matukio ya mauaji bado yanazidi kushamiri maeneo mbalimbali hapa nchini, ambapo mauaji ya kusikitisha yametokea katika kijiji cha Mashuba wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro. 

Imeripotiwa kuwa mwanamke ajulikanaye kwa jina la Grace Pius ameuawa kwa kuchinjwa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jana. 

Kwa mujibu wa shuhuda wetu aliyekuwepo eneo la tukio amesema baada ya kuzagaa tarifa hizo polisi walifika eneo la tukio kwa ajili ya upelelezi ikiwemo kuwasaka watuhumiwa wa mauaji hao.

Hadi sasa haijajulikana mara moja ni nini kimesababisha mwanamke huyo kuuawa kinyama namna hiyo. 

Hizi ni baadhi ya picha zikionesha nguo alizokuwa amezivaa marehemu kabla ya mauti kumfika huku zikiwa zina matone ya damu na alama za visu. 

Habari/Picha kwa mujibu wa mdau wetu kupitia whatsapp namba yetu +255 713 836 935
 




JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo