Habari ya mjini ni maandalizi kabambe ya harusi ya staa wa Bongo Fleva na Mbunge wa Viti Maalum (CCM) anayewakilisha Vijana Mkoa wa Geita, Vicky Pascal Kamata ikidaiwa kuwa shughuli hiyo itatafuna kiasi cha Sh. milioni 96.
Habari kutoka kwa chanzo cha ndani zinasema kuwa Vicky anatarajia
kufunga pingu za maisha Mei 24, mwaka huu na mchumba wake wa muda mrefu anayejulikana kwa jina la Charles Pai.
Imedaiwa kwamba mwanaume huyo ni kigogo ndani ya kampuni moja ya huduma za simu hapa nchini
