WANAUME RUKSA KUOA MKE ZAIDI YA MMOJA NCHINI KENYA

SHERIA inayoruhusu wanaume kuoa mke zaidi ya mmoja, imepitishwa nchini Kenya.

Rais Uhuru Kenyatta ametia saini sheria hiyo licha ya malalamiko kutoka kwa vikundi vya wanawake nchini humo.

Taarifa kutoka katika ofisi ya Rais ilisema kuwa mswada huo ambao unajumuisha vipengee kadhaa kuhusu ndoa , imekuwa sheria sasa.

Mswada huo ulioleta mageuzi katika sheria ya sasa , ulipitishwa na bunge mwezi jana kuidhinisha rasmi utamaduni wa ndoa ya zaidi ya mwanamke mmoja.

Taarifa ya Rais ilisema kuwa "ndoa ni muungano wa watu wawili mwanamke na mwanamume , ikiwa mume atataka kuoa mke mmoja au wawili, mwenyewe anapaswa kuamua.''

Mswada wa awali, ulimpa mwanamke haki ya kwenda mahakamani kupinga mume wake kuoa mke wa pili, lakini wabunge wanaume waliungana katika kuunga mkono mswada huo.
Wakati mswada huo ulipopitishwa mwezi jana, wabunge wanawake waliondoka bungeni kwa hasira baada ya mjadala mkali.

Shirikisho la kitaifa la mawakili wanawake pia limesema kuwa litapinga sheria hiyo mahakamani.
Katika sehemu nyingi barani Afrika, kuoa zaidi ya mwanamke mmoja ni jambo la kawaida katika tamaduni nyingi sawa na hali ilivyo nchini Kenya na hata pia miongoni mwa waumini wa dini ya kiisilamu.

Wengi wanasema kuwa sheria hiyo inapiga tu muhuri wa utamaduni uliopo.
Chanzo: BBC SWAHILI


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo