MWENYEKITI WA KIJIJI MATATANI KWA KULIMA MIHOGO MAKABURINI HUKO GEITA

Wananchi wa kijiji cha Bugulula katika kata ya Bugulula wiayani Geita mkoani Geita, wamemtaka mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana Bahati Matati kulirudisha shamba lao walilokuwa wakilitumia kwa ajili ya maziko baada ya kujimilikisha na kuanza kulima mihogo. 

Wakiongea kwa nyakati tofauti jana na waandishi wa habari wananchi hao wamesema wanashangaa kuona mwenyekiti wa kijiji hicho anachukua shamba hilo lililotengwa na wananchi kwenye mkutano wa serikali ya kijiji kwa ajili ya maziko.

Wananchi hao wameongeza kuwa kitendo cha mwenyekiti huyo kupora shamba hilo na kujimilikisha kinyume cha sheria, si cha kiungwana hivyo wameiomba serikali kuweza kulirudisha eneo hilo kwa wananchi ili liendelee na kazi iliyokusudiwa ya maziko. 

Kwa upande wake mwenyekiti huyo Bwana Matati, amesema shamba hilo ni mali yake na alipewa na uongozi wa serikali ya kijiji baada ya kuingia madarakani, na kuongeza kuwa hizo ni chuki kwa baadhi ya wananchi. 

Wananchi wa kijiji cha Bugulula wamekuwa na madai mengi na ya muda mrefu, kuhusu eneo hilo licha ya kupewa eneo lingine ambalo wanadai lina mawe hivyo hawawezi kuchimba umbali mrefu kwa ajili ya maziko.

Na Valence Robert - Geita


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo