MSANII DUDE AIBIWA NA VIBAKA

Stori: Gladness Mallya Via GPL.
MGANGA hajigangi! Licha ya kuwa msanii mahiri anayeelimisha jamii jinsi ya kugundua utapeli na kuepukana nao, Kulwa Kikumba ‘Dude’ ameibiwa ‘kupigwa’ vifaa vya saluni na vibaka.

Akistorisha na mwanahabari wetu, Dude alisema juzikati vibaka hao walipanda kwenye dari na kukata ‘celling board’ kisha kuingia ndani ya saluni yake hiyo ya kike inayosimamiwa na mkewe, maeneo ya Jeti-Lumo, Dar na kukomba vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni tatu na laki saba.

“Ukweli nimechoka sasa kila siku wananirudisha nyuma kimaendeleo kwa kuniibia sijui nifanyeje maana imeshakuwa hatari kwangu, wamechukua TV, madela, redio aina ya sabuufa na vingine vidogovidogo,” alisema Dude ambaye mwaka 2012 na 2013 aliwahi kulizwa vifaa mbalimbali vya nyumbani.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo