Na Erick Evarist
MWIGIZAJI ambaye ambaye alikuwa akifanya kazi kwa karibu sana na
marehemu Steven Kanumba, Mayasa Mrisho ‘Maya’ alijikuta akishindwa
kuhudhuria siku maalum ya marehemu baada ya kuzidiwa na ugonjwa wa
malaria.
Siku ya Kanumba Day iliadhimishwa Jumatatu iliyopita ambapo ndugu
pamoja na baadhi ya wasanii walijumuika pamoja kufanya maombi kanisani,
kwenda makaburini kumkumbuka marehemu kisha sherehe katika Ukumbi wa Dar
Live, Mbagala Zakhem, jijini Dar, lakini Maya alishindwa kutokana na
kuumwa huko.
“Nilizidiwa ghafla siku ya Jumapili, nikalazwa katika dispensari
ndogo hapa nyumbani Magomeni lakini baada ya kuanza dozi siku ile,
naendeleda vizuri, wameshaniruhusu,” alisema Maya.