MARADHI YALIYOMSIBU MAYA YAMPELEKEA KUSHINDWA KUSHIRIKI KUMBUKUMBU YA KIFO CHA KANUMBA

Na Erick Evarist
MWIGIZAJI ambaye ambaye alikuwa akifanya kazi kwa karibu sana na marehemu Steven Kanumba, Mayasa Mrisho ‘Maya’ alijikuta akishindwa kuhudhuria siku maalum ya marehemu baada ya kuzidiwa na ugonjwa wa malaria.

Siku ya Kanumba Day iliadhimishwa Jumatatu iliyopita ambapo ndugu pamoja na baadhi ya wasanii walijumuika pamoja kufanya maombi kanisani, kwenda makaburini kumkumbuka marehemu kisha sherehe katika Ukumbi wa Dar Live, Mbagala Zakhem, jijini Dar, lakini Maya alishindwa kutokana na kuumwa huko.

“Nilizidiwa ghafla siku ya Jumapili, nikalazwa katika dispensari ndogo hapa nyumbani Magomeni lakini baada ya kuanza dozi siku ile, naendeleda vizuri, wameshaniruhusu,” alisema Maya.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo