Kutokana na hali hiyo
Mkandarasi wa ujenzi huo atalazimika kuifumua na kuijenga upya barabara
hiyo ambayo ujenzi wake ulikamilika mapema mwaka huu.
Barabara ya
Meta kupitia kituo kikuu cha Mabasi cha jiji la Mbeya hadi mjini ni
miongoni mwa barabara kongwe zilizojengwa mwishoni mwa miaka ya 1970 na
tangu kipindi hicho haikuwahi kufanyiwa matengenezo makubwa zaidi ya
haya ya mwishoni mwa mwaka jana.
Kufumuliwa na kujengwa upya kwa
barabara hiyo kulikoigharimu serikali kiasi cha shilingi Bilioni 1.4
kupitia mfuko wa Brabara (Road Fund) kuliibua hisia za matuamani kwa
watumiaji wake na hasa wenye vyombo vya usafiri lakini matumaini hayo
yanayeyuka muda mfupi baada ya ujenzi huo
Wananchi hao wameenda
mbali zaidi kwa kuzilaumu mamlaka husika kwa kitendo cha kuyaruhusu
magari yenye uzito mkubwa kuingia katikati ya jiji huku zikijuwa kuwa
kufanya hivyo kunachangia uharibifu wa barabara.
