
Basi la timu ya Young Africans lililokuwa limebeba wachezaji pamoja na
viongozi wa benchi la ufundi limepata ajali eneo na Mikese Mizani mkoani Morogoro baada
ya Mabasi yaliyokua yakitanua kuelekea mikoa ya bara kuziba njia na
kusababisha kutumbukia kwenye mtaro.
Basi hilo limepata ajali likitokea
mkoani Morogoro kwenda Dar es Salaam baada ya mchezo wa Ligi Kuu Bara
dhidi ya Mtibwa Sugar uliopigwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro jana.
Taarifa zinasema Katika ajali hiyo iliyotokea majira ya saa tatu na nusu asubuhi hakuna
mtu yeyote aliyejeruhiwa na kwa sasa timu inaondoka na usafiri wa basi
jingine kuelekea jijini Dar es salaam.