PICHA ZA DARAJA LILILOSOMBWA NA MVUA RUVUMA

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akiwa katika daraja la Chimate ambalo mbao zake zimeoza na kupelekea kuhatarisha usalama kwa watumiaji wa daraja hilo katika Wialaya ya Nyasa, ambapo alitoa agizo kwa Meneja wa TANROADS mkoani humo kubadili mbao.
Pichani aliyesimama katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu akiwa katika daraja la kijiji cha Mbui ambacho daraja la mto Ng’ombo limesombwa na  maji na kukigawa kijiji hicho sehemu mbili,  sehemu moja ikiwa ina shule na sehemu moja kukiwa na zahanati.
Pichanini dereva wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma aliyejulikana kwa jina moja la Komba akitoa msaada wa kuwavusha watoto wa shule katika daraja la mto Mbui ambalo ni lamuda lililotengenezwa na wananchi wenyewe wa kijiji cha Ng’ombo.
Kuliani Mwenyekiti wa CCM, Mh. Oddo Mwisho akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu kuhusiana na daraja hilo lilisombwa na maji.
Wakazi wa kijiji cha Ng'ombo wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu ambaye hayupo pichani akiwataka wakazi hao kuwa na subira katika ujenzi wa daraja hilo kutokana na mto huo kuwa na tabia za kuhamahama.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo