Na Isabella Thomas - Dodoma
Katika hali ya kushangaza kwa kila
kipindi tunachoelekea msimu wa sikukuu kumekuwa na uhaba mkubwa wa
vitoweo hususani kuku katika maeneo mengi hasa ya mijini.
Hali hii
imejitokeza katika soko kuu la Majengo mjini Dodoma.
Kumekuwa na
upungufu wa kuku wanaouzwa kama kitoweo, hali hii imeonekena kwa kile
kinachodaiwa kuwa wafugaji wanaouza kuku kwa jumla wamewahifadhi kuku
hao huku wakilenga kuwauza katika sikukuu ya pasaka wiki tano zijazo kwa
lengo la kupata faida zaidi.
Hali hii pia imejitokeza ktk maeneo
mengine ya masoko madogo mjini Dodoma.
Kuku wakiwa wamehifadhiwa katika mabanda yao tayari kwa mauzo ya msimu wa sikukuu ya Pasaka wiki tano zijazo
PICHA NA MJENGWA BLOG