WAHITIMU WATAKIWA KUELIMISHA JAMII KUTANGAZA BIDHAA ZA TANZANIA


DSCF2810Kulia ni mgeni rasmi Adam Shayo,ambaye ni mkurugenzi wa Taasisi ya elimu ya Sila(SILA VOCATION TRUST ARUSHA) katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu katika  mahafali ya kwanza  chuo cha Biashara na Teknohama Arusha. kushoto ni mkurugenzi wa chuo hicho Valentune Ndanu
DSCF2801Meza kuu wakijiandaa kukabidhi vyeti kwa wahitimu 
DSCF2800Mgeni rasmi Bw. Adam Shayo akikabidhi cheti kwa mmoja wa wahitumu,wapili ni mkurugenzi wa chuo hicho Bw.Valentune Ndanu
DSCF2804Burudani nayo ilichukua sehemu yake
DSCF2797Baadhi ya waalikwa wakiwa wanaangalia burudani
DSCF2798Meza kuu wakijiandaa kukabidhi vyeti kwa wahitimu ngazi ya stashahada
DSCF2807Mgeni rasmi Bw. Adam Shayo katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu

Na Pamela Mollel,Arusha.

Wahitimu katika chuo cha Biashara na Teknohama Arusha(IBICTA)wametakiwa kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa kutafuta masoko nje ya nchi kwaajili ya kutangaza  bidhaa za Tanzania hali itakayo saidia  uchumi wa Taifa kuwa juu

Wito huo ulitolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Sila( SILA VOCATION TRUST ARUSHA) Bw. Adam Shayo juzi wakati alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya kwanza chuo cha Biashara na Teknohama Arusha

Alisema kuwa changamoto kubwa iliyopo ni pamoja na bidhaa za Tanzania kutotambulika katika soko la kimataifa huku akidai kuwa asilimia kubwa ya bidhaa zinazozalishwa hapa nchini zinaubora ukilinganisha na nchi zingine

Aidha aliwata wahitimu kutumia  stashahada zao katika kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kutafuta masoko nje ya nchi kwaajili ya bidhaa zinazozalishwa hapa Nchini

Kwa upande wake Mkurugenzi wa chuo hicho Bw.Valentune Ndanu alisema kuwa waliohitimu  katika chuo hicho ni wanafunzi 10 huku akidai kuwa elimu waliyoipata  wahitimu hao itawawezesha kufanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu 

Pia alitaja faida nyingine  watakayofaidika nayo ni pamoja na kutambua fursa  zilizopo sanjari na kujiingiza katika ujasiriamali hali itakayowasaidia kuwa na ajira ya kudumu

Malengo ya chuo hicho ni kutoa digrii ya biashara na teknohama hali itakayosaidia vijana kujiingiza katika ujasiriamali,


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo