VITUO VYA REDIO VYAASWA KUPIGA MIZIKI ISIYO NA MAADILI KWA JAMII

Ikiwa leo ni maadhimisho ya siku ya redio duniani, maadhimisho hayo kitaifa yamefanyika mkoani Dodoma ambapo redio zimeaswa kuacha tabia ya kupiga miziki isiyo na maadili kwa watanzania

Rai hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt. rehema Nchimbi ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo wakati akizungumza kwenye ukumbi wa Dodoma Hotel

Pia Dkt Nchimbi amekemea watangazaji kuacha matamshi yanayowafanya wanawake kuacha kusikiliza redio kwani nao wana haki ya kusikiliza redio

kauli mbiu ya mwaka huu ni "tusherehekee ushiriki wa wanawake katika redio na wote wanaowawezesha"

Na Veronica Mtauka, Dodoma.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo