Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana katika eneo la Sogea, mji mdogo wa Tunduma wilayani Momba.
Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Ahmed Msangi, aliwataja waliopoteza
maisha kuwa ni baba wa familia hiyo, Steven Mwaijombe (35), mkewe Ester
Kibona (25) pamoja na mtoto wao Edga Mwaijombe (2), wakazi wa Sogea.
Alisema miili ya marehemu imehifadhiwa katika kituo cha afya Tunduma kwa ajili ya taratibu za mazishi.
Wakati huohuo, watu saba wanashikiliwa na polisi mkoani hapa kwa
kukutwa na pombe haramu aina ya gongo yenye ujazo wa lita 1.5.
Watuhumiwa hao walikamatwa wakiwa wanakunywa pombe hiyo kutokana na
msako wa kukamata watu wanaofanya biashara hiyo mkoani hapa.
Kamanda Msangi alisema taratibu za kuwafikisha mahakamani zinafanyika.