MBUNGE WA CCM NI MGONJWA, HALI TETE ICU..!!!



Bwanamdogo, Saidi Ramadhani [CCM]
Chalinze Constituency

Habari zisizo njema kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano ni kwamba mbunge wa Chalinze Mh. Said Bwanamdogo anaumwa hoi mahututi akiwa amelazwa katika chumba maalumu kwa wagonjwa wanaopewa uangalizi maalum (ICU) MOI.

Chanzo cha habari hizi kiliwashuhudia baadhi ya wabunge wa mkoa wa pwani wakiwa pale MOI kumjulia hali mwenzao. Wabunge walioonekana maeneo hayo ni pamoja na Dr Seif Rashid Rufiji na naibu waziri wa afya pamoja na Mh Koka mbunge wa Kibaha mjini.

Duru za uhakika zinaeleza kuwa Mh Bwanamdogo amekuwa mgonjwa kwa kipindi kirefu na juhudi za kupelekwa nje ya nchi kwa matibabu bado hazikuzaa matunda mpaka kufikia uamuzi wa kumrudisha nchini.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo