MAMA MLEMAVU AJERUHIWA VIBAYA NA KUFANYIWA VITENDO VYA KIKATILI


Na Ibrahim Yassin,Kyela

KATIKA hari isiyokuwa ya kawaida kijana Razaro Mwabakiugwe mkazi wa kijiji cha Lupembe kata ya Ikolo wilayani Kyela mkoani Mbeya anatafutwa na Polisi kwa tuhuma za kumfanyia ukatili Lucia Katule ambaye ni mlemavu kwa kumshambulia kwa makonde na kumsababishia maumivu makali sehemu ya mwili wake.

Akisimulia mkasa huo mbele ya waandishi wa habari nyumbani kwake Katuli alisema kuwa tukio hilo lililtokea jana majira ya saa sita mchana katika kitongoji cha Mikoroshoni kata ya kyela mjini baada ya kijana huyo kuingia na baiskeli katika varanda ya nyumba wanayoishi na alianzisha fujo hizo baada ya wapangaji wenzake kumhoji.

Alisema kuwa kijana baada ya kuhojiwa kuhusu kitendo cha kuigia na baiskeli ndani ya varanda alijibu kwa kejeli kuwa mbona mlemavu anaingia na baiskeli humu lakini hamumsemi na kuwa alizidi kuongea kashfa ya kuwa ndiyo maana idi amaini alikuwa anawatupa baharini watu kama hawa.

Aliongeza kuwa baada ya kusema hivyo alishuka kwenye baiskei na kuanza kumshambulia kwa ngumi na mateke hadi kumsababishia maumivu makali ikiwamo kumuumiza mguu wake wa kushoto bila kujali ulemavu alionao.

Aliendelea kusema kuwa baada ya hapo wasamalia wema walimuokoa na kumkibiza katika kituo cha polisi wilaya ambao walimpatia RB Iliyomuwezesha kwenda kupata matibabu katika hospitali ya wilaya ya Kyela ambapo alitibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Mikoroshoni Kalison Bongo alisema alikiri kuwepo na tukio hilo na kudai kuwa alifuatwa na wasamalia wema ofisini kwake na kujurishwa tukio hilo ambapo alifika eneo la tukio kwe lengo la kupata ufumbuzi juu ya tukio hilo.

Alisema alipofika katika nyumba hiyo hakumkuta mtu na ndipo wapangaji wengine walimueleza kuwa mama aliyeshambuliwa alikimbizwa hospitalini na kijana aliyeshambulia amekimbilia kusiko julikana mara baada ya kufanya kosa hilo na kuwa alitoa maagizo kuwa iwapo atakuja afike katika ofisi yake. ndani ya siku tatu.

Aliongeza kuwa iwapo hatafika katika ofisi yake ndani ya siku tatu ataungana na jeshi la polisi kwa ajili ya kumsaka popote alipo ili afikishwe katika mikono ya sheria ili aweze kuadabishwa kwa mujibu wa sheria na itakuwa ni fundisho kwa vijana wengine wenyetabia kama hiyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo