DIAMOND NA HAMISA MOBETO WADAIWA KUWA NA UHUSIANO WA KIMAPENZI, WEMA ASHAURIWA KULIVUA PENDO




Hamisa Hassan Mobeto ambaye ni model na actress anayekimbiza katika tasnia ya filamu nchini anadaiwa kuwa mapenzini na Diamond Platinumz a.k.a Sukari ya warembo huku uhusiano wao ukidaiwa kuwa wa muda mrefu.....

Chanzo kimoja kilichodai kuwa karibu na Hamisa ambaye alishawahi kushiriki  katika  mashindano  ya  Miss Tanzania kiliuambia mtandao wa Swahiliworld  kuwa   Hamisa na Diamond  ni  wapenzi  wa  muda  mrefu  na  kwamba  Wema  Sepetu  hana  lake  kwa  Diamond:
 
 "Hivi mnajua kuwa Diamond anawachanganya kwa wakati mmoja Wema na Hamisa Mobeto?, Hamisa na Diamond ni wapenzi wa muda mrefu sana lakini  wanafanya siri...Hamisa anamwangalia tu Wema akiwewesekea penzi la Diamond huku yeye akijilia kivyake".Kilisema  chanzo  hicho
 
Hamisa alipotafutwa ili kutolea ufafanuzi madai hayo hakuweza kupatikana  mara  moja.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo