Taarifa zilizoufikia mtandao huu hivi ppunde kutoka kwa mdau wetu wa EDDY BLOG Arusha, ni kwamba ndege ya Ethiopian Airlines iliyokuwa imetua kwa dharura uwanja mdogo wa ndege Arusha na kusababisha ndege hiyo kukwama kwenye tope na nyasi, hii leo majira ya saa tano na dakika arobaini na tano, imeruka kuelekea uwanja wa ndege wa Kilimanjaro (KIA)
Hii inafuatia juhudi za kuinasua ndege hiyo zilofanywa toka jana kuzaa matunda
Asante sana mdau wetu kwa taarifa hiyo
