DEREVA WA BASI LA HOOD LILILOPATA AJALI LEO MOROGORO APONGEZWA NA ABIRIA

Basi la Kampuni ya Hood Limited lenye namba za usajili T 159 AXM lililokuwa linatoka Mbeya kuelekea Arusha limepinduka katika eneo la Melela- Mlandizi, Mvomero mkoani Morogoro mchana wa leo na kuua mtu mmoja huku likiwaacha majeruhi kadhaa.

Imeelezwa kuwa basi hilo lilipinduka wakati dereva akilikwepa lori lililokuwa likijaribu kulipita gari jingine kwenye kona: ‘Mimi nilikuwa natoka Mbeya naenda Moshi kwa ajli ya sikukuu ya Krismas, dereva wetu amefanya kazi kubwa sana ya kuokoa maisha yetu. 

Tulipofika hapa kwenye kona, dereva wetu baada ya kuona lori limejaa upande wetu akaamua kukwepa kugongana nalo uso kwa uso na kuingia huku lilipo. Binafsi nampa pongezi nyingi dereva wa hili basi letu,” abiria Bi. Ruth Mwambogoso amenukuliwa na GPL akisema hayo.

Picha zifuatazo ni kwa hisani ya Dunstan Shekidele wa GPL.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo