Naibu spika Job Ndugai asubuhi hii ameitaka serikali kuharakisha kuleta taarifa kamili bungeni endapo daraja sifuri limefutwa na kuwekwa daraja la tano badala ya sifuri ama la
Mh Ndugai ametoa kauli hiyo kufuatia mbunge wa Kawe mh. Halima Mdee kuomba muongozo wa spika kufuatia kauli za kukanganya zinazotolewa na viongozi wa wizara ya elimu
Ndugai amesema ni vyema serikali ikatoa taarifa ya ufafanuzi wa suala hilo haraka iwezekanavyo kwa kuwa wanafunzi wa kidato cha nne wanaendelea na mitihani ya kidato cha nne sasa, hivyo si vizuri wanafunzi hao wakaendelea kufanya mitihani ilihali hawajui mpangilio wa madaraja ukoje kwa kuwa kila mtu anatoa taarifa yake
Waziri wa sera, uratibu na bunge William Lukuvi amelihakikishia bunge kuwa serikali itatoa taarifa hiyo mapema ambayo anaimani itatoa mkanganyiko huo