WATU wawili wamepoteza maisha baada ya kudondoka kwenye shimo la choo
lililokuwa wazi eneo la Kibamba Hospitali, jijini Dar es Salaam!
Mmoja
kati ya marehemu hao alikuwa akijenga ghorofa ndipo alipoteleza na
kutumbukia katika shimo hilo lenye maji ambalo litatumika kama choo cha
ghorofa hilo.
Baada ya tukio hilo, rafiki yake alijaribu kumuokoa fundi
huyo lakini kwa bahati mbaya naye alitumbukia shimoni humo na wote
wawili kupoteza maisha.
Mmoja wa marehemu hao ametambulika kwa jina moja
la Bakari.
Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahala pema peponi. Amen!
-GPL-