Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akizungumza na wananchi wa
Kisiwa cha Tumbatu katika hafla ya uzinduzi wa Kituo cha Matangazo ya
Redio Jamii Kisiwani humo.
Na. Othman Khamis Ame
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema Vituo vya
Redio Jamii hapa Nchini vinapaswa kuwa chem Chem ya elimu itakayotoa
manufaa kwa Jamii inayovizunguuka Vituo hivyo badala ya utaratibu wa
kurusha vipindi vya muziki wakati wote.
Kauli
hiyo aliitoa wakati akiizindua Redio Jamii ya Wilaya ndogo ya Tumbatu
hapo katika jengo la Wilaya hiyo liliopo katika Kijiji cha Kichangani
ikiwa ni muendelezo wa shamra shamra za maadhimisho ya kutimia miaka 50
ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.
Balozi
Seif alisema mijadala na nakala zinazohusiana na masuala ya Uchumi,
siasa, jamii na Maendeleo ndio lengo lililokusudiwa katika uanzishwaji
wa Redio hizo na kupelekea kuungwa mkono na Taasisi na mashirika ya
maendeleo Duniani.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwataka watendaji wa Redio Jamii Tumbatu
kujitahidi kuwaelimisha wananchi kuhusu uvuvi bora na mambo mengi
yanayohusiana na bahari kwani maisha ya wananchi hao yametegemea zaidi
sekta ya bahari.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akikata utepe kuzindua
rasmi Redio Jamii ya Wilaya ndogo ya Tumbatu visiwani Zanzibar. Kushoto
ni Kaimu Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Elimu, Sayansi na Mawasiliano
ya Umoja wa Mataifa (Unesco)Bw. Abdul Wahab Coulibaly wanaofadhili
unzishwaji wa redio za jamii Tanzania Bara na Visiwani.
Mkurugenzi
wa Kituo cha Redio Jamii cha Tumbatu Ali Khamis Mtwana akimpatia
maelezo juu ya utendaji wa Kituo hicho Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi mara baada ya kukizindua rasmi.
Kulia
kwa Balozi Seif ni Kaimu Mwakilishi Mkazi wa Unesco Bw. Abdul Wahab
Coulibaly na Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Mh. Said Ali
Mbaouk.
Mkurugenzi
wa Kituo cha Redio Jamii cha Tumbatu Ali Khamis Mtwana akifanya vitu
vyake wakati akiwa hewani kurusha matangazo ya kituo cha Redio Jamii
Tumbatu mara baada ya kuzinduliwa na Balozi Seif Ali Iddi. Kushoto kwa
Balozi Sefu ni Kaimu Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Elimu, Sayansi na
Mawasiliano ya Umoja wa Mataifa (Unesco)Bw. Abdul Wahab Coulibaly
wafadhili wa mradi huo.(Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ na Zainul Mzige wa MOblog).