POLISI WAUA MAGAIDI WAWILI WALIOVAMIA MSIKITI KILINDI TANGA

Watu wawili wanaodaiwa kuhusishwa na vitendo vya kigaidi wameuawa kwa kupigwa risasi wakati kundi hilo lilipokuwa msikitini huku wafuasi wake wakiwa na silaha za moto na baridi walipokuwa wakijibizana kwa kutumia silaha mbali mbali ndipo askari walipowahi kuwashambulia viongozi wa kundi hilo kisha kuwanyang'anya silaha zao ili kuepuka madhara makubwa zaidi.

Mkuu wa mkoa wa Tanga luteni mstaafu Chiku Gallawa amesema tukio hilo limetokea katika kijiji cha Kimamba kilichopo kata ya Negero wilayani Kilindi wakati kundi hilo lilipokuwa limejiandaa kujibu mashambulizi ya askari msikitini kwa kuwa na silaha aina ya bunduki na mapanga ndipo viongozi hao waliposhambuliwa ambapo mmoja alifariki papo hapo huku mwingine akifariki hospitali ya wilaya.

Chanzo: ITV


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo