WASANII WENGI WAJITOKEZA SHINDANO LA TUSKER PROJECT FAME

Waandaaji wa shindano la kusaka vipaji vya uimbaji la tusker project fame wameelezea kufurahishwa na mwitikio wa wasanii mbalimbali waliojitokeza katika usaili kwa ajili ya kuwania nafasi ya kuiwakilisha tanzania kwenye mashindano hayo.

Zaidi ya wasanii 150 wamejitokeza katika usaili uliofanyika jijini dar es salaam ambapo kutokana na vipaji vya hali ya juu vilivyooneshwa na wasanii hao majaji wamekuwa na kazi ngumu ya kuchagua wasanii watatu tu kati yao ambao watapeperusha bendera ya tanzania katika mashindano ya tusker project fame huku pia yakishirikisha washiriki kutoka kenya, uganda, sudan kusini na burundi.
 
Nao baadhi ya wasanii waliopata fursa ya kuzungumza na itv wamesema mashindano hayo yatawasaidia kuinua vipaji vyao ikiwa watapata fursa ya kuingia kwenye jumba la tusker project fame hivyo wamewaomba sapoti ya watanzania katika kila hatua watakayofikia kupitia mashindano hayo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo