| Wakazi wa mji wa Iringa wakiwa katika semina ya kamata Fursa leo |
| Mwakilishi wa Max malipo akitoa maelezo ya jinsi walivyokuza ajira nchini |
Mmoja kati ya wawezeshaji katika
semina ya kamata Fursa inayoendeshwa na kituo cha radio Clouds Fm
,msanii Nickson simon a.k.a Nikki wa pili wa pili akieleza fursa
zilizopo na changamoto zake.
...................................................
...................................................
MSANII Nickson simon a.k.a Nikki wa pili
amewataka vijana nchini
kuepuka kukimbilia mijini na badala yake kutumia
fursa zilizopo katika maeneo
yao kama
njia ya kujikwamua kiuchumi.
Kwani alisema kuwa lengo La
semina hiyo ya kamata
Fursa imelenga kubadili
mitizamo ya jamii
hasa vijana katika
kuwawezesha kubadili mitizamo
yao ili kuweza kujipatia maendeleo .
Msanii Nikki wa pili
ameyasema hayo leo katika
ukumbi wa st.Dominic
katika warsha ya
siku moja ya kamata
fursa iliyoandaliwa na kituo
bora cha radio
Clouds Fm
Alisema kuwa mbali
ya viongozi wa kada
mbali mbali kuzungumzia suala la
fursa ila bado watanzania waliowengi bado hawajabahatika kuiona
fursa hiyo.
Hivyo alisema kuwa
warsha hiyo imelenga pia
kuwawezesha watanzania kuanza
kuziona fursa zilizopo
na ikibidi kuweza kuzitumia fursa
hizo.
“ Tunapinga mawazo
ya vijana ambao
wanatoka vijijini na kukimbilia mijini kwenda
kutafuta fursa mbali
mbali huku wakiwa
wameacha fursa zilizopo katika maeneo
yao ambayo wanaishi”
Hata hivyo amesema baada
kuzunguka katika maeneo mbali
mbali ya nchini ikiwemo Kigoma , Tabora ,Mtwara
, Mbeya na Iringa
wamebaini kuwa tatizo
kubwa ni thamani
ndogo ya mazao
yanazozalishwa katika maeneo hayo.
Mbali ya kutaka
thamani ya mazao hayo
kuongezwa bado alisema
sehemu kubwa ya
wazalishaji mali ni wazee
huku vijana wengi
wamekuwa wakikimbilia mijini
na kuwa iwapo wataongeza
thamani ya mazao kuna
uwezekano wa vijana wengi
kuepuka kukimbilia mjini
“ Vijana lazima
kufanya tafiti ili kuona
ni namna gani unaweza kupata
bei ya bidhaa mbali mbali na baada ya
hapo kujiunga katika vikundi
vya kiuchumi ili kuweza
kupata mikopo “
Pia alisema zipo
taasisi nyingi ambazo
zinatoa mikopo katika makundi mbali mbali
na moja kati ya taasisi hizo ni
pamoja na NSSF ambao wanatoa
mikopo ya zaidi ya Tsh bilioni 1 katika
vikundi.
chanzo: mzee wa matukio daima