MWANAUME ASIMULIA JINSI MKEWE ALIVYOMLAZIMISHA KUNYWA SUMU

 Charles Mbaruku Kimani
MWANAMUME mmoja kaunti ya Murang’a alinusurika kifo baada ya mkewe kumlazimisha kunywa sumu.
Bw Charles Mbaruku Kimani kutoka kijiji cha Matongu katika lokesheni ya Kimathi eneo la Kiharu KENYA alidai mkewe alimpiga dafrau usiku na kutaka kumnywesha sumu kwa nguvu lakini akakataa.

Akiongea na Taifa Leo Ijumaa katika kituo cha polisi mjini Murang’a ambapo aliandikisha ripoti, jamaa huyo wa miaka 54 alidai mkewe ana mazoea ya kumshambulia akishirikiana na mwanawe wa kiume.

Bw Kimani alisema wameoana kwa miaka 13 na wamekuwa wakizozana kwa siku nyingi huku mkewe akitoroka kwa wazazi wake mara kadhaa katika kijiji cha Kimicha kaunti jirani ya Kirinyaga.

Alisema kuwa siku ya Jumamosi usiku, mkewe alichanganya dawa ya kuua kupe na kuitia kwenye chupa na kumkaba koo mzee huyo huku akitaka anywe dawa hiyo ili afe.

“Tulikuwa tumetoka safari na ndani ya nyumba kulikuwa na giza kwani hatukuwa tumewasha taa na nilikuwa nimeketi  kitini wakati mke wangu aliponishambulia,” alisema Bw Kimani ambaye alitibiwa hospitali kuu ya Murang’a baada ya kisa hicho.

Mwanamme huyo ambaye anafanya biashara ya kuuza changarawe alidai mkewe alimshika kwenye sehemu ya shingo na kuelekeza chupa hiyo iliyojaa sumu kwenye mdomo wake lakini mwanamme huyo akamuuma mkewe mkono wakati wa kisa hicho


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo