MSANII WA SIKU NYINGI RAS LION AZUNGUMZIA ALIPO KWA SASA

Najua wengi mmemmisi msanii huyu na mnazikumbuka kazi zake ikiwemo (Umaskini huu) kazi ilomzolea kitita cha mashabiki Ndani na nje ya nchi.. 
 
Kwa sasa msanii huyu amekaa kimya kwa mda mrefu kidogo baada ya kuachia kazi iliotambulika kwa jina la (Sumu ya panya) aliamua kujichimbia na kuendelea kufanya maandalizi ya kulipa deni kwa mashabiki wake yani kuwapa burudani na ujumbe kama ilivyo ada, 
 
Akiongea na mwandishi wetu hakutaka kufunguka sana kuhusu ujio wake wa sasa bali alizungumza kwa ufupi tu kwamba kuna vitu anaviandaa yeye na mwenzie ''Joni woka'' yani kwa ujumla kundi lao la (WA2KU2) Linaloundwa na wasanii wawili ''Ras Lion'' na ''Joni woka'' sasa lipo katika maandalizi ya kazi kali hivyo mashabiki wasijali wasubiri burudani.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo