MALORI YA MIZIGO ZAIDI YA 400 KUTOKA TANZANIA YAENDELEA NA SAFARI RWANDA

Zaidi ya magari ya mizigo 400 yaliyokuwa yamekwama katika eneo la  Rusumo mpaka wa Tanzania na nchi ya Rwanda baada ya serikali ya Rwanda  kupandisha kodi ya kutoka dola 152 hadi dola 500 kwa kila gari moja la mizigo na kusababisha msongamano mkubwa mpakani

Hapo  yameanza kupita kufuatia tozo hiyo mpya kusitishwa  ambapo magari mengi yanapita Rwanda kwenda Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Wakizungumza kabla ya kuruhusiwa baadhi ya madereva wa magari ya mizigo wameiomba serikali ya Rwanda kufanya makubaliano na nchi wanachama wa afrika mashariki kwa kuwa na lugha moja ya kodi na kwamba marumbano yaliyopo kati ya rais wa nchi ya Rwanda na Tanzania na kwamba rais wa Rwanda amepandisha gharama bila taarifa kwa wasafirishaji hali inayosababisha usumbufu kwa madereva.

Kwa upandewake mmoja wa watendaji wa serikali wa Mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) aliopo katika eneo la mpaka wa tanzania na nchi ya Rwanda Bw. Nasoro Ibrahimu amekili kuwepo kwa msongamano mkubwa wa magari ya mizigo katika eneo la tanzania baada ya kuzuiliwa kuingia katika nchi ya Rwanda hali iliyosababisha kufunga barabara ya rusumo ngara isipitike

CHANZO: ITV


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo