HOTUBA YA WAZIRI MKUU PINDA AKITOA HOJA YA KUAHIRISHA BUNGE LEO 06.09.2013

HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE, DODOMA TAREHE 06 SEPTEMBA, 2013

I.      UTANGULIZI:

a)            Maswali
                                                                                        
1.            Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kutekeleza na kukamilisha majukumu yetu katika muda uliopangwa. Katika Mkutano huu Maswali 120 ya Msingi na 305 ya Nyongeza ya Waheshimiwa Wabunge yalijibiwa na Serikali. Aidha, jumla ya Maswali 12 ya Msingi ya Papo kwa Papo na 11 ya Nyongeza yalijibiwa na Waziri Mkuu.
b)           Miswada

2.            Mheshimiwa Spika, katika Mkutano huu, Bunge lako Tukufu lilijadili na kupitisha Miswada Mitatu (3). Miswada hiyo ni:
i)             Muswada wa Sheria ya Taifa ya Umwagiliaji wa Mwaka 2013 [The National Irrigation Bill, 2013];

ii)            Muswada wa Sheria wa Vyama vya Ushirika wa Mwaka 2013 [The Cooperative Societies Bill, 2013]; na

iii)           Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2013 [The Constitutional Review (Amendment) Bill, 2013].

3.            Mheshimiwa Spika, napenda nitumie nafasi hii kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa kujadili na kukubali kupitisha Miswada hiyo kwa umahiri mkubwa. Aidha, niwapongeze Mawaziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na Wataalam wote waliohusika na Maandalizi ya Miswada hiyo. Kipekee niwashukuru Wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge kwa kupitia Miswada yote na kutoa maoni yao, ambayo sehemu kubwa yamezingatiwa na Serikali katika kuboresha Miswada hiyo.

4.            Mheshimiwa Spika, asubuhi ya leo Bunge lako Tukufu lilipokea Kauli za Mawaziri wa Fedha na Uchukuzi. Wote tunawashukuru kwa maelezo yao.

II.            UTEKELEZAJI WA MFUMO WA MATOKEO MAKUBWA SASA “BIG RESULTS NOW”

  ENDELEA KWA KUBOFYA HAPA>>>>>>>>>>>>


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo