TAMASHA kubwa na la kipekee la Dar Filamu Festival (DFF) linatarajia
kuonyesha filamu zaidi ya 20 katika viwanja vya CoICT- UDSM- Posta
Kijitonyama kuanzia tarehe 24 September 2013 , filamu zitachaguliwa
kutoka filamu zaidi ya mia mbili ziliomba kuonyeshwa na wamiliki wa
filamu hizo kazi zitakazoonyeshwa zitakuwa zile zilizopendekezwa na bodi
ya DFF.
Akiongea na FC mkurugenzi wa Haak Neel Production Godfrey katula amesema filamu zitakazoonyeshwa ni zile ambazo zimeonekana kupendwa na kukidhi vitu mbalimbali kama maadili utamaduni, ubora wa filamu (Quality), sauti nzuri filamu zilipitia katika taasisi husika pia kutakuwa na kazi zilizofanya vizuri sokoni.
“Dar Filamu Festival ni tamasha linalowakutanisha wadau wa filamu nchini kwa kujadili masuala ya tasnia ya filamu, lakini pia ni wakati wa kujitangaza kupitia kazi hizo, jambo lingine ni kuleta mwamko wa wapenzi wa filamu kujenga utamaduni wa kuangalia filamu katika majumba ya sinema yaliyokuwepo,”anasema Goddy.
Tamasha la Filamu la Dar Filamu Festival (DFF), litaanza rasmi tarehe 24/September/2013 hadi tarehe 26 kwa kila siku filamu zitaanza kuruka saa 12 jioni hadi saa sita usiku ulinzi wa kutosha kutoka kwa makampuni ya kimataifa wakishirikiana na Polisi huku filamu hizo zikirushwa kupitia Projector kubwa One air mtazamaji akipata filamu safi bila kufinya macho kwani utaiona live.
CHANZO:FC
Akiongea na FC mkurugenzi wa Haak Neel Production Godfrey katula amesema filamu zitakazoonyeshwa ni zile ambazo zimeonekana kupendwa na kukidhi vitu mbalimbali kama maadili utamaduni, ubora wa filamu (Quality), sauti nzuri filamu zilipitia katika taasisi husika pia kutakuwa na kazi zilizofanya vizuri sokoni.
“Dar Filamu Festival ni tamasha linalowakutanisha wadau wa filamu nchini kwa kujadili masuala ya tasnia ya filamu, lakini pia ni wakati wa kujitangaza kupitia kazi hizo, jambo lingine ni kuleta mwamko wa wapenzi wa filamu kujenga utamaduni wa kuangalia filamu katika majumba ya sinema yaliyokuwepo,”anasema Goddy.
Tamasha la Filamu la Dar Filamu Festival (DFF), litaanza rasmi tarehe 24/September/2013 hadi tarehe 26 kwa kila siku filamu zitaanza kuruka saa 12 jioni hadi saa sita usiku ulinzi wa kutosha kutoka kwa makampuni ya kimataifa wakishirikiana na Polisi huku filamu hizo zikirushwa kupitia Projector kubwa One air mtazamaji akipata filamu safi bila kufinya macho kwani utaiona live.
CHANZO:FC