WAZIRI MKUU PINDA ASHTAKIWA MAHAKAMA KUU

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na TLC leo wamemshtaki  Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mwanasheria mkuu wa serikali kwa kukiuka Katiba katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Kesi iliofunguliwa katika Mahakama Kuu ni ya kikatiba. Kesi hiyo inasubiri kupangiwa majaji.

Kesi hiyo imefunguliwa katika mahakama hiyo ikiwa ni hatua za kisheria kupinga kauli alioitoa Pinda bungeni hivi karibuni kwamba watakaokiukwa amri za vyombo vya dola ‘wapigwe tu’.

Hivi karibuni Waziri Mkuu, Pinda akiwa bungeni alisema serikali imechoshwa na vurugu zinazotokea mara kwa mara na kwamba hakuna namna nyingine ya kuwadhibiti raia wanaowadhuru vyombo vya dola na kutotii amri zaidi ya kuwapiga.

Awali LHRC ilisema Pinda anapaswa kushtakiwa kwa kuwa amevunja kifungu cha katiba ya Usawa mbele ya sheria  ibara 13 (1).
 
Mkurugenzi wa Maboresho na Utetezi wa  LHRC, Harold Sungusia alitoa kauli hiyo mapema wiki hii wakati akitoa ripoti ya utafiti ya miezi sita kuhusu mambo mbalimbali yanayolenga haki za binadamu.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo