WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA ATOA MSAADA WA MASHINE YA KUFULIA KWA KITUO CHA KULELEA MAYATIMA CHA KATANDALA MKOANI RUKWA

Mashine maalum ya kufulia nguo aina ya HITACHI iliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Pinda kwa kituo cha kulelea mayatima cha Katandala Mkoani Rukwa na kukabidhiwa kituoni hapo na Katibu wake wa Jimbo Ndugu Charles Kanyanda leo tarehe 30, Agosti 2013. Msaada huo wenye thamani ya Tshs. Milioni moja na nusu (1.5) ni ahadi ya Waziri Mkuu aliyoitoa alipotembelea kituoni hapo mapema mwaka huu.
Ndudu Charles Kanyanda Katibu wa Jimbo wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Katavi akimkabidhi Mama Mkuu Mariastella Wampembe wa Masista Maria Mtakatifu Malkia wa Afika ambao ni wamiliki wa kituo cha kulelea mayatima cha Katandala mashine maalum ya kufulia nguo iliyotolewa na Waziri Mkuu kwa kituo hicho leo tarehe 30, Agosti 2013. 
Mama Mkuu Mariastella Wampembe wa Masista Maria Mtakatifu Malkia wa Afika wamiliki wa kituo cha kulea mayatima cha Katandala Mkoani Rukwa akitoa shukrani zake za dhati kwa Waziri Mkuu kupitia kwa Katibu wake wa Jimbo Ndugu Charles Kanyanda kwa msaada huo wa mashine ya kufulia. (Picha na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa)


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo