SHUTUMA NZITO WIZARA YA MIUNDOMBINU ZANZIBAR, SPIKA AAHIRISHA MJADALA

 
Kutokana na wajumbe wa baraza la wawakilishi kutoa shtuma nzito juu ya utendaji wa wizara ya mindombinu na mawasiliano ya Zanzibar ,spika wa baraza la wawakilishi ameamua kuahirisha mjadala wa wizara hiyo ili kuwapa muda zaidi waziri  na watendaji wake kujipanga  na kuja na majibu ya uhakika.
 
Hatua hiyo imekuja baada ya wajumbe wa baraza hilo kutoka CCM na CUF wapatao zaidi ya 50 kuchangia hotuba ya bajeti ya wizara hiyo iliyowasilishwa na waziri wa miundombinu na mawasiliano Mhe Rashid Seif, ambapo karibu wajumbe wote walikuwa wakali na kutoridhika na utendaji wa wizara hiyo katika masuala ya utawala,ujenzi wa viwanja vya ndege na uimarishaji na ujenzi wa barabara za Unguja na Pemba ,usafiri wa baharini ambapo wajumbe waliweka misimamo yao  ya kuzuia vifungu na kutoa shilingi wakati wamajumuisho.
 
Kutokana na hoja hizo za wawakilishi Spika alisogeza mbele mjadala huo na kuamua wizara ya biashara kuwasilisha bajeti yake huku waziri wa mindombinu anatarajiwa kujibu hoja za wawakilishi baada ya wizara ya biashara kumaliza uwasilishaji wake.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo