JESHI LA POLISI NCHINI LAPOKEA MSAADA WA GARI MAALUM LENYE MITAMBO YA UPELELEZI

Jeshi la polisi nchini limepokea msaada wa gari maalum lenye mitambo itayoweza kufanya upelelezi,ukaguzi na uchunguzi wa kitaalam utakaosaidia kupata ushahidi wa uhakika katika kupambana na matukio ya uhalifu hapa nchini.
 
Akiziungumza na waandishi wa habari, baada ya kusaini hati za ushirikianao wa jeshi la polisi la Uturuki na kisha kukabidhiwa gari hilo, mkuu wa jeshi la polisi nchini,insepekta jenerali Saidi Mwema amesema baadhi ya wahalifu wamekuwa wakihachiwa huru na mahakama kwa sababu ya ushahidi wa jeshi la polisi kutokamilika kutokana kutokuwepo na vifaa vya kitaalam ambapo  amesisitiza vifaa vilivyomo katika gari hilo vitasaidia kukusanya taarifa za uhakika za matukio ya uhalifu.
 
Naibu mkurugenzi wa jeshi la polisi la taifa la uturuki bwana Zeki Gakatalilaya amesema makubalino ya ulinzi ni moja ya njia ya kushirikiana yatakayosaidia majeshi la polisi katika nchi hizo mbali,ambapo amesema tayari serikali ya Uturuki inashirikiana na nchi zaidi ya tisa katika maswala ya usalama.
 
Naibu katibu mkuu wa wizara ya mambo ya ndani bibi Mwamini Malemi amesema kukabidhiwa kwa gari hilo ni mwendelezo wa makubaliano kati ya rais Jakaya Kikwete na rais wa Uturuki ya kuendeleza jeshi la polisi la Tanzania na Uturuki katika kuangalia matukio ya kiharifu na kufanya uchunguzi wa kitaalam na kuondokana na tatizo la ushahidi kutokakamilika kwenye vyombo vya utoaji haki.
 
 chanzo:itv


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo