RAIS UHURU KENYATTA AKUTANA NA RAIS MSTAAFU DANIEL ARAP MOI IKULU

Uhuru na Moi
Rais Uhuru Kenyatta akutana na Rais Mstaafu Daniel arap Moi ikulu, Nairobi Agosti 1, 2013. Walishauriana kuhusu mikakati ya kudumisha amani Afrika Mashariki na eneo la Maziwa Makuu. Picha/PSCU
=======

RAIS Uhuru Kenyatta Alhamisi Hii alikutana na kushauriana na Rais Mstaafu Daniel arap Moi ikulu, Nairobi. Wawili hao walishauriana kuhusu mikakati ya kudumisha amani Afrika Mashariki na eneo la Maziwa Makuu.
Mkutano wao ulijiri siku moja tu baada ya viongozi wa Afrika Mashariki na Maziwa Makuu kukutana Gigiri, Nairobi kwa Kongamano la Kimataifa Kuhusu eneo la Maziwa Makuu (ICGLR).

Mkutano huo ulijadili mizozo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Sudan.

Baada ya mkutano huo, viongozi hao waliunga mkono mashauriano kati ya serikali ya DR Congo na waasi wa M23 yaliyofanikishwa na Uganda na kutaka pande zote ziendelee na mashauriano hayo.

Pia walizitaka Uganda na Sudan Kusini ziendelee kuheshimu makubaliano ya kudumisha amani.

Waliohudhuria kongamano hilo ni pamoja na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Rais  Michel A.M. Nondokro Djotodia wa Jamhuri ya Afrika ya Kati.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo