POLISI WAWAPOKONYA WAVUVI SAMAKI ZAO

Migingo
Kisiwa cha Migingo.

MAAFISA wa usalama kutoka Uganda kwa mara nyingine waliwapokonya samaki wavuvi wa Kenya katika Ziwa la Victoria.
Waliwapokonya wavuvi hao kilo 1,000 za samaki wa thamani ya Sh200,000 katika ufuo wa Mugabo kaunti ya Migori Jumanne jioni.

Raia wa Uganda walidai kuwa wavuvi hao walikuwa wameingia katika sehemu yao ya ziwa bila ruhusa.

Maafisa hao waliokuwa wamejihami waliwazuilia wavuvi hao waliokuwa bado ndani ya ziwa na kuwapokonya samaki hao huku wakiwatishia kwa bunduki. 

Mkuu wa Wilaya ya Nyatike Moses Ivuto alisema Maafisa wa serikali ya Kenya watakutana na wenzao wa Uganda ili kujadiliana kuhusu mzozo huo wa uvuvi. 

“Tutaenda kujadiliana kuhusu suluhu ya mizozo ambayo imeendelea kuhusisha ziwa hili,” alisema.

Wavuvi wa Kenya walidai kuwa samaki wanaopokonywa huuziwa bwenyenye mmoja kutoka Uganda.

Wiki moja iliyopita, maafisa wa Uganda walitoroka na tani mbili za samaki yenye thamani ya Sh500,000 kutoka kwa wavuvi wa Kenya.

Maafisa hao ambao wamekita kambi katika kisiwa tata cha Migingo waliwapokonya wavuvi hao samaki huku wakiwatisha kwa bunduki.

Mwenyekiti wa Usimamizi wa Uvuvi katika kisiwa cha Migingo Juma Ombori alisema maafisa hao waliojihami waliwavamia wavuvi hao wakati walikuwa wanarejea kuvua samaki majira ya usiku.

Gavana wa kaunti ya Migori Okoth Obado alitoa wito kwa serikali ya Uganda kuheshimu Wakenya. 

Alisema RaisYoweri Museveni anapaswa kuwaondoa maafisa wake wa usalama kutoka kisima hicho kama njia ya kudumisha ujirani mwema na Kenya. 

“Nimeongea na Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake  William Ruto kuhusu mzozo wa Migingo na wote wawili wamenihakikishia kuwa serikali inashughulikia jambo hilo kwa haraka,” Bw Obado aliwaambia waandishi wa habari.

Mzozo wa kisiwa cha Migingo ulianza 2009 nchi zote mbili zikingangania kukimiliki. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo