RAIS KENYATTA AFUTA OFISI YA MSEMAJI WA SERIKALI YAKE

RAIS Uhuru Kenyatta amevunja ofisi ya Msemaji wa Serikali ambayo ilibuniwa na Rais Mtsaafu Mwai Kibaki. Bw Muthui Kariuki aliyekuwa Msemaji wa Serikali sasa atapewa kazi nyingine serikalini.
Taarifa kutoka Ikulu ilisema hatua hiyo imechukuliwa ili kulainisha mawasiliano kutoka kwa serikali.

“Ofisi ya Katibu wa Mawasiliano ya Umma na Msemaji wa Serikali haiingiani na muundo mpya wa utawala wa Rais Uhuru Kenyatta na imevunjwa,” ilisema taarifa ya PSCU.

Msemaji wa Ikulu Manoah Esipisu atatekeleza majukumu yaliyokuwa yakitekelezwa na msemaji wa serikali kwa mujibu wa taarifa hiyo.

Dkt Alfred Mutua alikuwa wa kwanza kuhudumu katika wadhifa huo na akarithiwa na Bw Kariuki. Bw Kariuki aliteuliwa na Rais Mstaafu Kibaki kabla ya kustaafu kwake.

Dkt Mutua kwa sasa ndiye gavana wa Kaunti ya Machakos.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo