POLISI WADAIWA KUMSHAMBULIA MWANANCHI KWA KIPIGO HADI KUMVUNJA MKONO

Akionesha Jeraha alilopata baada ya kipigo.
 

Jeshi la polisi mkoani ruvuma limeingia lawamani baada ya askari wake kudaiwa kumshambulia, Bwana Omary Hamis mkazi wa Mfaranyaki Makaburini na kumvunja mara mbili mkono wa kulia na bega la kushoto na kumjeruhi maeneo mbalimbali ya mwili wake baada ya kupigana na mkewe ambapo amelazwa katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma kwa matibabu.

Askari wa jeshi hilo wanadaiwa kumshambulia  bw. Omary Hamis mkazi wa Mfaranyaki Songea huku watoto wake wakishuhudia na kumpiga kwa virungu na kumvunja mkono wa  kulia na bega la kushoto na kumsababishia majeraha mbambali kwenye mwili wake baada ya  mwananchi huyo kupigana na mkewe aliyewapigia simu polisi kutokana ugomvi waliokuwa nao mke na mume. 

Mtoto wa bw. Abubakary Omary mwenye miaka 11 alishudia tukio hilo wakati baba yake ikipata kipigo hicho.

Kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma bw. George Chiposi alipofuatwa ofisini kwake kwa siku mbili mfululizo aweze kuzungumzia tukio hilo hakuweza kupatikana na alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi na kuelezwa kuhusiana na tukio hilo hakusema chohote na kukata simu.

NA Joseph Mwambije, Songea


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo