KAGAME ASHAURIWA KUSIKILIZA USHAURI WA KIKWETE

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Dk. Richard Sezibera, ametoa kauli ya kumtaka Rais wa Rwanda, Paul Kagame kutumia busara kwa kusikiliza ushauri wa kidiplomasia aliopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Kikwete kwa sababu ushauri huo umezingatia maslahi ya nchi ya Rwanda na wananchi wake kwa ujumla.

Dr. Richard Sezibera alisema inampasa Rais Kagame aache kutoa maneno ya kashfa dhidi ya Rais Kikwete na asichukulie kwa kuwa Rais Kikwete yuko kimya basi inamaanisha amekubaliana na kashfa zake na za wanyarwanda, isipokuwa Rais Kikwete anatumia busara ambayo ni muhimu sana kwa usalama wa ukanda huu wa Afrika.

Aliendelea kuisifu Tanzania kwani pamoja na dhihaka inayotolewa na Rais Kagame dhidi ya Rais Kikwete, hakuna lolote mbaya ambalo Tanzania imelifanya kuathiri utendaji kazi wa wafanyakazi wa ofisi za Makao Makuu ya Jumuiya jijini Arusha. Wanyarwanda waliopo hapa wanaendelea na kazi zao bila kubughudhiwa jambo ambalo linaonyesha uungwana wa Tanzania.

Dr. Richard Sezibera aliyasema hayo jijini Arusha alipokuwa anaongea na waandishi wa habari kuhusu uendeshaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo