Ng’ombe zaidi ya 80 wameuawa kikatili kwa kukatwakatwa mapanga
na wengine kuchinjwa baada ya kuingia katika mashamba ya wakulima wa
Vijiji vya Kisara na Mbogo, Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro.
Tukio hilo ambalo liliamsha hasira kwa wamiliki wa
ng’ombe hao lilitokea Agosti 19 katika vijiji hivyo maeneo ya
mashambani na kwamba tukio hilo limefanywa na watu wasiojulikana ambao
wanadhaniwa kuwa ni wakulima wenye mashamba katika vijiji hivyo.
Ng’ombe wengine walikuwa wamevunjwa miguu na hivyo
kushindwa kutembea ambapo wamiliki wa ng’ombe hao waliwashutumu
wakulima kwa kuchukua sheria mkononi na hivyo kuiomba Serikali kuchukua
hatua zinazostahiki ikiwa ni pamoja kuwasaka waliohusika katika tukio
hilo.
Nao baadhi ya wakulima wilayani humo walionyeshwa
kusikitishwa na tukio hilo .huku wakiiomba Serikali kuhakikisha inapanga
mipango mizuri ili kunusuru migogoro ya wakulima na wafuagaji ambayo
inaweza kusababisha machafuko kwenye vijiji.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Anthony Mtaka alisema kuwa Serikali ya Wilaya imeanza kuchukua hatua kwa kushirikiana na polisi ili waliohusika katika tukio hilo waweze kuwakamata na kuchukuliwa hatua za kisheria.
CHANZO:MWANANCHI
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Anthony Mtaka alisema kuwa Serikali ya Wilaya imeanza kuchukua hatua kwa kushirikiana na polisi ili waliohusika katika tukio hilo waweze kuwakamata na kuchukuliwa hatua za kisheria.
CHANZO:MWANANCHI