MWENYEKITI WA CHADEMA FREEMAN MBOWE NA WENZAKE WAKAMATWA NA POLISI IRINGA

Mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowe, wabunge Tundu Lissu, Peter Msigwa, Joseph Mbilinyi (Sugu), David Silinde na viongozi wengine wa mkoa na Wilaya ya Iringa mjini, akiwemo Diwani Nyalusi, wanashikiliwa na Jeshi la Polisi, Kituo Kikuu Iringa, kwa kosa la kuzidisha muda wa mkutano.

Polisi wanasema mkutano ulimalizika saa 12.30 badala ya saa 12.00 jioni


Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Jeshi la Polisi, zote hazizungumzii muda maalumu wa kufunga mkutano, bali sun set (kuzama kwa jua). 

Kwa sababu kuzama kwa jua inategemea hali ya jiografia ya eneo hilo. Maeneo kama Kigoma saa 1 jioni, jua linawaka kama vile saa 12.

Ni Sheria ya Uchaguzi pekee, ndiyo inazungumzia muda maalum ambao ni 12.30. Na ni kwa sababu ya mazingira ya equality kwa ajili ya wagombea wote kufanya kampeni ndani ya muda mmoja.


Tutaendelea kuwajuza zaidi kuhusu hili.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo