Msichana mmoja
ambaye jina lake halikujulika amejikukuta katika wakati mgumu baada ya
kuzomewa na kuchapwa viboko na kundi la watu katika eneo la soko la NMC jiji Arusha kwa madai ya kuvaa nguo fupi hali iliyowalazimu
wasamaria wema kuingilia kati na kutumia nguvu kubwa ili kumwokoa na
kumsitiri kwa kumfunika na nguo zingine.
Mwandishi wetu Halfani Lihundi kutoka Arusha
alikuwapo katika sakata hilo na ametuma taarifa hii iliyosema, watu
walio shuhudia tukio hilo wamesema wamechukizwa na aina ya nguo
alizizovaa msichana huyo ambazo haziendani na maadili ya Kitanzania,
ndiyo maana wameamua kumwadabisha ili kukomesha tabia hiyo.
Kwa upande wao wanawake waliyo msitiri msichana huyo
kwa kumpa nguo za heshima na kumhifadhi katika Gareji ya jirani kabla ya
kumkimbiza kwa gari aina ya Toyota Hiace wamesema hawaridhishwi na
tabia hiyo inayowadhalilisha wanawake na kuwataka wasichana kuavaa nguo
za kujisitiri ili kujenga heshima katika jamii.
na itv