MBUNGE WA MAKETE DK BINILITH MAHENGE AWAHAKIKISHIA WANANCHI WA KATA YA KITULO KUWA UMEME UTAWAKA DESEMBA MWAKA HUU

Wananchi wa kata ya kitulo wilaya ya Makete mkoani Njombe wamehakikishiwa kupata umeme na maji ifikapo Desemba mwaka huu

Kauli hiyo imetolewa na mbunge wa jimbo la Makete ambaye pia ni naibu waziri wa maji Dk Binilith Mahenge katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo katani hapo

Dk Mahenge amesema tayari transfoma ya kwa ajili ya umeme wa kata hiyo imeshapatikana na ipo katika ofisi za tanesco wilaya ya Makete na itafungwa mwezi huu hivyo waondoe shaka

"Najua tabu mnazozipata kwenye suala zima la umeme hapa Kitulo lakini litakwisha hivi karibuni maana mwezi huu Tanesco watakuja kufunga transfoma hapa na taratibu zingine zifuate lakini hadi desemba mwaka huu umeme lazima uwake" alisema Mahenge

Kwa upande wa maji amesema tayari mkandarasi ameanza kutengeneza inteki (njia ya maji) ili wananchi waanze kupata maji ya bomba baada ya kupata adha ya ukosefu wa maji kwa muda mrefu

Nao wananchi wa kata hiyo wamesema wamefurahishwa na maneno hayo na kumtaka mbunge kufuatilia masuala hayo kwa makini huku wakimpongeza kwa kuwatembelea na kusikiliza kero zao na kuzipatia majibu

Na Riziki Manfred


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo