MAHAKAMA YAMWACHIA HURU MBUNGE WA MTWARA MJINI

 Murji(3)-1
Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Mtwara imemfutia shtaka la kesi ya uchochezi iliyokuwa ikimkabili Mbunge wa Mtwara Mjini (CCM) Hassnein Murji.

Katika mahakama hiyo wakili anayemtetea mbunge huyo Peter Kibatala aliiomba mahakama kuifuta kesi hiyo ambayo ilisomwa Julai 3, mwaka huu kwa madai kwamba hati ya mashtaka haionyeshi ni makosa yapi mtuhumiwa aliyatenda kabla ya kukamatwa.

Murji alifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo akikabiliwa na kesi ya uchochezi baada ya kudaiwa kufanya makosa hayo Januari 19, mwaka huu katika eneo la Ligula mkoani hapa.

Kutokana na hoja ya wakili Kibatala, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Dynes Lyimo alifuta shtaka hilo na kumwachia mshtakiwa huru.


CHANZO:habarimasai.com


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo