MADUKA MTAA WA SAMORA YABOMOLEWA HUKU BIDHAA ZIKIWA NDANI

 
Barabara ya Samora katikati ya jiji la Dar es Salaam imefungwa kwa saa kadhaa huku jeshi la polisi likiimarisha ulinzi katika maeneo yote ya mtaa huo ili kufanikisha zoezi la kuwaondoa wapangaji waliokuwa wakiishi katika baadhi ya nyumba za shirika la nyumba la taifa zilizopo katika mtaa huo.
 
Zoezi la kuwaondoa wapangaji hao katika nyumba hizo ambazo ni mali ya shirika la nyumba la taifa ilianza tangu saa 12 asubuhi sambamba na zoezi la ubomoaji uliofanywa na tingatinga huku zoezi hilo likisimamiwa na askari wa jeshi la polisi ili kuakikisha linafanikiwa  kama hivi.

Baadhi ya wapangaji hao,akiwemo bwana  Anely Chawda na Bi Debora Kamboge, wamelalamikia uongozi wa shirika la nyumba la taifa kwa kukiuka mkataba waliowapa kwa kusema mkataba huo ulitakiwa kuisha mwezi Novemba mwaka huu kwa mujibu wa mkataba wa shirika la nyumba la taifa walivyoandika wenyewe,lakini cha kusikitisha zaidi ni kwamba mpaka mwezi huu wa August 2013 walilipa kodi katika shirika hilo na ikapokelewa na risiti wanazo lakini wameondolewa katika nyumba hizo bila kujua wataenda  kuishi wapi na shughuli zao watafanyia wapi.

Wakala wa shirika hilo bwana Joshua Mwaituka, aliyekuwepo eneo la tukio, alionekana kuzingirwa na baadhi ya wapangaji hao kwa lengo la kuhoji kwa nini hawakupewa muda wa kutosha ili kuondoa mali zao kiustarabu na  badala yake zoezi hilo kufanyika nyakati za sikukuu ambapo asilimia kubwa ya wapangaji hao hawapo,hali iliyochangia baadhi ya vibaka kutaka kuiba na kuambulia kipigo.

Kutokana na malalamiko hayo kuwa makubwa ikiwemo wapangaji kusitishwa mikataba yao pamoja na kuondolewa katika nyumba  wakati wamelipa kodi hadi mwezi huu,ITV ilimtafuta mkurugenzi wa shirika la nyumba la taifa bwana Nehemia Mchechu na kusema shirika hilo halina nia mbaya ya kumwibia mtu hivyo waliolipa kodi zao wafike ofisini kwao na watarejeshewa na kwamba walichokifanya ni jambo jema la kuwaondoa watu katika nyumba hatarishi na pia wametii maagizo ya mahakama.
 
NA ITV


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo