Imeripotiwa
kutoka London – Uingereza kuwa mabinti wawili ambao walimwagiwa
tindikali Kisiwani Unguja ambapo walikwenda kama wafanyakazi wa
kujitolea kufundisha kiingereza mashuleni wanaendelea vizuri.
Kwa sasa mabinti hao wanatibiwa katika hospitali ijulikanayo kwa jina la Chelsea and Westminster ambayo imebobea kwenye kutibu matatizo yanayotokana na kuunguzwa mjini London.
Mama yake Katie, mmoja wa majeruhi hao, ajulikanaye kwa jina la Nicky Gee amesema familia zao zimekuwa zinapitia katika kipindi kigumu sana kufuatia unyama ambao mabinti wao wametendewa wakati wakiwa wanafanya shughuli za kujitolea visiwani Zanzibar.
Kwa sasa mabinti hao wanatibiwa katika hospitali ijulikanayo kwa jina la Chelsea and Westminster ambayo imebobea kwenye kutibu matatizo yanayotokana na kuunguzwa mjini London.
Mama yake Katie, mmoja wa majeruhi hao, ajulikanaye kwa jina la Nicky Gee amesema familia zao zimekuwa zinapitia katika kipindi kigumu sana kufuatia unyama ambao mabinti wao wametendewa wakati wakiwa wanafanya shughuli za kujitolea visiwani Zanzibar.