KIMENUKA BUNGENI,MH.MWIGULU NCHEMBA AWALIPUA MBOWE NA DR.SLAA KWA MAUAJI


Ni kiongozi jasiri,ni kiongozi mzalendo,nikijana shupavu,amejitolea kuipigania Tanzania ya kweli,amejitolea kupambana na wahujumu wa nchi popote pale Tanzania,Ni Mh.Mwigulu lameck Nchemba leo tena anafanya kile CHADEMA wapata maumivu yasiyonakifani,Mwigulu nchemba amewalipua kisawa sawa Vioongozi wa CHADEMA wa juu wakiongozwa na Freeman aikael Mbowe na Dr.slaa kuhusika na umwagaji damu za Watanzania wasio na hatia. 

Ni siku leo asubuhi kwenye kipindi cha Maswali na majibu,Mh.Mwigulu Nchemba akitoa swali la nyongeza anasema "Ndani ya miaka miwili CHADEMA wakiongozwa na Freeman Mbowe na Dr.slaa wamesababisha vifo Arusha,Ndago,Morogopro na Iringa.

Kwa mauaji haya yaliyotokana na ukatili wao na kutojali maisha ya watu kwa viongozi hawa wa CHADEMA.

Mbowe na Slaa wanastahili kuwa JELA na walistahili kuwa jela siku nyingi".

Anasema Mbunge wa Iramba Magharibi.Baada ya kauli hiyo Ukumbi wa bunge unalindima kwa makofi mazito.Huku upande wa CHADEMA kila mmoja akiishia kukunja sura.

chanzo: jamii forum


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo