JUMA KASEJA ANASWA AKIFANYA MAZOEZI NA MTIBWA SUGAR

KIPA namba moja wa timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' aliyekuwa mlinda mlango wa kutumainiwa wa klabu ya Simba SC, Juma Kaseja, leo asubuhi ameungana na wachezaji wa Mtibwa Sugar kufanya mazoezi kwenye Uwanja wa Chuo cha Ustawi wa Jamii uliopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Katika mazoezi hayo Kaseja alikutana na mshambuliaji Musa Hassan Mgosi ambaye aliwahi kucheza naye Simba SC.

Mgosi kwa sasa ni mchezaji wa Mtibwa Sugar wakati Kaseja bado hatma yake haijafahamika baada ya kuachana na Simba msimu uliopita.

(PICHA NA RICHARD BUKOS / GPL)


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo