FFU WASHINDWA KUWATAWANYA WAFANYAKAZI WA TAZARA WALIOGOMA

Jaribio la kuwatawanya wafanyakazi wa shirika la reli Tanzania na Zambia (TAZARA) waliopo katika mgomo ulioingia siku ya nne kwa kutumia kikosi cha askari wa kutuliza ghasia (FFU) limegonga mwamba baada ya askari hao kufika eneo la tukio na kukaa kimya huku wakiwa na mabomu ya machozi na muda mfupi kutoweka bila kufanya chochote.

Wafanyakazi hao ambao walikuwa wamesimama nje ya jengo la TAZARA baada ya kuzuiliwa kuingia ndani huku baadhi ya maeneo yakiwa yamezungushiwa ribon za polisi kuashiria kuwa watu hawaruhusiwa kuingia eneo hilo, wafanyakazi hao wamelalamikia kitendo hicho na kudai kuwa kimewadhalilisha na kudai kuwa mgomo huo utaendelea hadi watakapolipwa haki zao.

Mgomo huo umesababisha abiria waliokuwa wanasafiri kwa treni ya Tazara kuendelea kukwama katika stesheni hiyo ambapo ITV imeshuhudia baadhi ya abiria wakiwa kituoni hapo wakisubiri hatima ya safari zao huku baadhi ya maofisa wakiendelea kukatisha tiketi ilihali wakijua uwezekano wa kusafiri haupo.

Mmoja wa viongozi wa wafanyakazi hao Bw Mussa Kalala amesema zoezi la mgomo bado litaendelea na alipoulizwa hatua zilizochukuliwa na wahusika wa tazara tangu waanze mgomo huo amesema hakuna kiongozi yeyote wa utawala wameonana naye isipokuwa wamebandikiwa tu matangazo yanayodai kuwa watalipwa mishahara yao agost 29 mwaka huu.

Kufuatia sakata hilo itv imeutafuta uongozi wa Tazara ili kulitolea ufafanuzi suala hilo ambapo afisa uhusiano wa Tazara Mkoa wa Tanzania Bi Regina Tarimo mbali na kukiri kuwa madai yao ni ya kweli pia amesema tatizo hilo kwa sasa linashughulikiwa na serikali zote mbili tanzania na Zambia.
 
chanzo:itv


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo