ASASI YA SSCSA YATUMIA MIL 41 KATIKA MPANGO MKAKATI WA MWAKA MMOJA.

 
ZAIDI ya shilingi milioni 41 zimetumika katika shughuli za maendeleo kwa kipindi cha mwaka mmoja katika utekelezaji wa mpango mkakati wa asasi isiyo kuwa ya kiserikali ya The Struggle for suppot Community Alliance (SSCSA) Pambana Saidia Jamii wilayani Kyela

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo  mwenyekiti mtendaji wa asasi hiyo Abrahamu Mwanyamaki amesema kuwa asasi hiyo ilizindua mpango wake mkakati wa miaka mitano februari mwaka jana ukilenga kutumia zaidi ya bilioni 2 na kuwa kwa kipindi cha mwaka mmoja wameweza kutumia kiasi hicho cha fedha katika kukamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo

Alisema kuwa asasi  hiyo ambayo usajiri wake ni wa kitaifa na makao yake makuu yakiwa wilayani Kyela imeweza kufanya upembuzi yakinifu na kubaini matatizo kadhaa yanayoikabili jamii na kwamba kwa kuanzia wilayani kyela amebaini kuwapo kwa changamoto kadhaa ambazo asasi yake imeanza nazo

Alisema kimsingi huduma za kijamii zinatekelezwa na serikali lakini kutokana na serikali kuwa na mambo mengi asasi za kijamii kama hiyo uisaidia serikali katika kutatua baadhi ya changamoto zinazoikabili jamii hii ya Watanzania

Mwenyekiti huyo mtendaji alisema kuanzia katika kipindi cha Februari hadi Augost mwaka huu asasi yake imeweza kusaidia kutoa madawati 100 katika shule ya msingi ya Ikombe,saruji kwa shule ya msingi malungo,mabati katika msikiti mkuu wa wilaya,mbegu ya matikiti na madawa kwa wajasiliamali wa kata ya Lusungo,Mchanga kwa ajili ya ujenzi wa hosteli ya walimu kata ya Makwale.

Misaada mingine ni katika ujenzi wa makanisa na misikiti,kuchangia ununuzi wa vyombo vya kisasa vya mziki katika makanisa mbalimbali,msaada wa fedha kwa Wahanga wa mafuriko katika kijiji cha Ngereka kata ya Makwale ambapo mto uliacha njia yake ya asili na kuharibu makazi ya watu,mashamba na kanisa la KKKT na eneo la maziko.

Pia asasi hiyo imefadhili ligi itakayoshirikisha timu mbalimbali katika vijiji na kata zote za wilaya Kyela na lengo ni kutaka kuifanya jamii kujengeka kiafya na kuacha kujiingiza katika makundi mbalimbali yasiyofaa na kupata muda wa kukutana na watu tofauti na kubadiishana mawazo namna ya kujiletea maendeleo

Mwanyamaki alidai kuwa licha ya kufanya yote hayo lakini amekuwa akikabiliana na changamoto kubwa kutoka kwa wanasiasa na kuwa shughuli zinazofanywa na asasi hiyo ni za kijamii na wala haziusiani kabisa na mambo ya kisiasa na kuwa hilo halitaikwamisha asasi yake kuendelea na shughuli zake za kuisaidia jamii
 
Na Ibrahim Yassin


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo